Mapigano kati ya makundi pinzani ya Libya mashariki mwa Tripoli yameingia siku ya pili jana

In Kimataifa
Mapigano kati ya makundi pinzani ya Libya mashariki mwa Tripoli yameingia siku ya pili jana, na kuwazuia wakaazi kurejea majumbani kwao.
Mapigano yalizuka Jumapili wakati makundi yenye silaha yanayoipinga serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa mjini Tripoli yalijaribu kuingia katika mji huo mkuu na wakakabiliwa na makundi hasimu ambayo yanaegemea upande wa serikali hiyo.
Wizara ya afya ya Libya imethibitisha kuwa karibu watu wanne wameuawa na wengine 21 wamejeruhiwa katika mapigano hayo.
 Serikali ya Umoja wa Kitaifa imeshindwa kuweka utulivu tangu ilipowasili mjini Tripoli Machi mwaka jana. Serikali hiyo inapingwa na makundi ambayo yanadhibiti mashariki mwa Libya, ambako kamanda wa kijeshi Khalifa Haftar amekuwa akiimarisha nafasi yake kwa kuwateua mameya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu