Mapigano kati ya makundi pinzani ya Libya mashariki mwa Tripoli yameingia siku ya pili jana

In Kimataifa
Mapigano kati ya makundi pinzani ya Libya mashariki mwa Tripoli yameingia siku ya pili jana, na kuwazuia wakaazi kurejea majumbani kwao.
Mapigano yalizuka Jumapili wakati makundi yenye silaha yanayoipinga serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa mjini Tripoli yalijaribu kuingia katika mji huo mkuu na wakakabiliwa na makundi hasimu ambayo yanaegemea upande wa serikali hiyo.
Wizara ya afya ya Libya imethibitisha kuwa karibu watu wanne wameuawa na wengine 21 wamejeruhiwa katika mapigano hayo.
 Serikali ya Umoja wa Kitaifa imeshindwa kuweka utulivu tangu ilipowasili mjini Tripoli Machi mwaka jana. Serikali hiyo inapingwa na makundi ambayo yanadhibiti mashariki mwa Libya, ambako kamanda wa kijeshi Khalifa Haftar amekuwa akiimarisha nafasi yake kwa kuwateua mameya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu