Marekani kuondoa wasiwasi kwa Uturuki kuwapatia silaha wapiganaji wa kikundi nchini Syria.

In Kimataifa

Waziri wa ulinzi wa Marekani Jim Mattis amesema leo kwamba anaimani Marekani inaweza kuondoa wasi wasi wowote wa Uturuki kuhusiana na uamuzi wa kuwapatia silaha wapiganaji wa Kikundi nchini Syria ambao Uturuki inawaona kama magaidi.

Mattis amesema katika mkutano na waandishi habari nchini Lithuania kwamba serikali yake itafanyakazi kwa karibu na Uturuki kusaidia usalama wao katika mpaka wa kusini.

Wakati huo huo wapiganaji wa Kikurdi nchini Syria wamekaribisha tangazo la serikali ya rais Trump kwamba, itawapatia silaha nzito ili kupambana na kundi la Dola la Kiislamu, lakini Uturuki imesema kila silaha itakayotolewa kwa kundi hilo ni kitisho kwa nchi yake.

Mzozo huo unaweza kuzusha mapigano zaidi baina ya washirika hao muhimu wa Marekani katika mapambano dhidi ya kundi la Dola la Kiislamu wakati kundi hilo la Wakurdi wa Syria linajitayarisha kwa operesheni kubwa kuwaondoa wanamgambo wa IS kutoka ngome yao ya mwisho katika mji wa Raqa.

Wakati huo huo Mattis amesema Marekani na NATO ziko tayari kuweka vifaa muhimu vinavyohitajika, kusaidia kuongeza mfumo wa ulinzi katika mataifa ya eneo

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu