Marekani yaichunguza Cuba.

In Kimataifa

Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Marekani inachunguza ripoti za matukio ya kushangaza ambayo yamewaathiri Wamarekani 16 wanaoishi Cuba.

Ripoti kadhaa za vyombo vya habari zimedokeza kuwa huenda walikuwa waathiriwa wa kile kinachifahamika kama “shambulizi la kutumia kifaa cha sauti”.

Maafisa wanasema raia wa Marekani wanaofanya kazi katika ubalozi wa nchi hiyo mjini Havana wamekumbwa na dalili za kimwili zinazosababishwa na “matukio” yasiyotambulika ambayo yalianza mwishoni mwa mwaka wa 2016.

Wafanyakazi kadhaa walirejeshwa nyumbani Marekani kutokana na matatizo ya kusikia na madhara mengine. Kwa mujibu wa televisheni ya CBS, madhara hayo ni pamoja na kichefuchefu, matatizo ya kutoweza kusimama vizuri na hata kuumia kwa ubongo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu