Marekani yaiwekea vikwazo benki moja ya China

In Kimataifa
China imeghadhabishwa sana na hatua ya Marekani ya kuiwekea vikwazo benki moja ya China ambayo inatuhumuwa kuhusika katika utakatishaji wa fedha za Korea Kaskazini.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya taifa hilo ameitaka Marekani “kukoma kuchukua hatua zisizo sahihi” kuepusha kudhuru ushirikiano baina ya nchi hizo.
Marekani ilitangaza hatua hiyo, pamoja na vikwazo dhidi ya kampuni ya uchukuzi wa meli ya China na raia wawili wa China mnamo Alhamisi.
Imesema lengo la vikwazo hivyo ni kupunguza fedha ambazo Korea Kaskazini ,inaweza kutumia kuendeleza mpango wake wa kustawisha silaha.
Umoja wa Mataifa ulikuwa tayari umeiwekea Korea Kaskazini msururu wa vikwazo, lakini China inatazamwa na wengi kama taifa lililo na uwezo zaidi wa kuiyumbisha Korea Kaskazini kupitia vikwazo vya kiuchumi.
Washington imekuwa ikiishinikiza Beijing kuchukua hatua kali zaidi hasa kutokana na hatua ya Pyongyang ya kufanyia majaribio makombora ya masafa marefu.
Lakini kupitia Twitter mapema mwezi huu, Rais Donald Trump amesema hatua ambazo China imechukua kufikia sasa hazijatosha.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu