Masaa 4 ya mahojiano ya Lowassa na DCI haya hapa.

In Kitaifa

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amehojiwa kwa zaidi ya saa 4 na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kwa tuhuma za uchochezi.

Lowassa amehojiwa jana Dar es Salaam katika Makao Makuu ya Polisi kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 8:14 mchana, kwa kile alichodai kuwa ni kutokana na hotuba aliyoitoa Jumamosi katika Jimbo la Ukonga lililo chini ya Mbunge, Mwita Waitara.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya mahojiano hayo, Lowassa amesema kuwa baada ya mahojiano hayo, anatakiwa kuripoti tena katika ofisi hizo kesho saa 6 mchana.

Aidha, amesema kuwa wapo katika utekelezaji wa ilani ya chama hicho na kwamba wanachama wake wawe na amani, kwani mambo yako safi na ameitwa kwa nia njema.

Wakili wa Lowassa, Peter Kibatala amesema walipokea mwito kutoka kwa DCI ukimtaka aripoti saa 4 jana ambapo ameeleza kuwa Lowassa anadaiwa kutoa maneno ya kichochezi Juni 23, mwaka huu katika futari iliyoandaliwa na Waitara.

Naye Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji alisema walioruhusiwa kuingia ndani kwenye mahojiano ni Lowassa na wanasheria wake na kwamba wao walikuwa nje kama watazamaji.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu