MASHIRIKA manne ya kimataifa kwa pamoja jana yalielezea kuunga mkono kampeni ya kitaifa ya usafi ijulikanayo kama Niko Tayari inayoendeshwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

In Kitaifa

MASHIRIKA manne ya kimataifa kwa pamoja jana yalielezea kuunga mkono kampeni ya kitaifa ya usafi ijulikanayo kama Niko Tayari inayoendeshwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Mashirika hayo ni UNICEF (Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto), Benki ya Dunia, Shirika la misaada la Uingereza (DFID), Shirika la Miradi la Ujerumani (GIZ) na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA).

Mashirika hayo ya maendeleo ambayo wawakilishi wake walikutana jana jijini Dar es Salaam, yamekubali kuunga mkono kampeni hiyo iliyozinduliwa mwezi uliopita mjini Dodoma. Kampeni hiyo imelenga kuhamasisha usafi wa mazingira kwa kila Mtanzania hasa kuwa na choo katika kila familia na kujenga utamaduni wa kunawa mikono.

Akizungumza jana, Mratibu wa kampeni ya Nipo Tayari, Anyitike Mwakitalima kutoka Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, alisema ili kuwa na huduma bora ya maji, usafi wa mazingira ni muhimu kuzingatiwa.

Kampeni hiyo ya usafi wa mazingira na matumizi bora ya choo (NikoTayari) inatarajiwa kuwa chachu ya upatikanaji wa maji safi na salama na kuboresha afya za Watanzania wote, mijini na vijijini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu