Mashirika ya kutetea haki za binadamu yaungana kutaka shitaka dhidi ya kiongozi wa upinzani nchini Zambia kufutiliwa mbali.

In Kimataifa

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty limeungana na mashirika mengine yanayotaka shitaka la uhaini dhidi ya kiongozi wa upinzani nchini Zambia na wenzake watano kufutiliwa mbali mara moja na kusema, ni kampeni ya mateso .Hakainde Hichilema alikamatwa baada ya kukataa kuupisha njia msafara wa rais Edgar Lungu,Kitendo kinachoonekana kama utovu wa adabu kwa rais.

Hakainde pamoja na wenzie watano ambao ni wajumbe wa chama cha United Party for National Development wamekuwa wakishikiliwa kwa zaidi wiki mbili kwa kile Amnesty ilichosema ni kosa la usalama wa barabarani na sio uhaini.

Pia Amnesty imetaka kuchunguzwa kwa tuhuma za kuteswa kwa kiongozi huyo na watu waliokuwa wamejifunika nyuso.Mashtaka ya uhaini yanaonekana kama njia moja wapo ya rais ya kunyamazisha upinzani, baada ya uchaguzi uliopingwa ambao uliambatana na vurugu.

Kwa upande wake, kiongozi huyo wa upinzani amekuwa akijitetea kwamba waliruhusiwa kuupita msafara wa rais na mamlaka kwa sababu walikuwa wakienda kwenye shughuli ya kidini

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu