Masikitiko shambulizi la kigaidi London

In Kimataifa
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May anasema shambulizi la kigaidi nje ya msikiti Kaskazini mwa jiji London, linasikitisha na kuchosha.
Shambulizi hilo limesababisha kifo cha mtu mmoja na zaidi ya 10 kujeruhiwa.
Waliojeruhiwa wanaendelea kupata matibabu hospitalini.
Bi. May amesema kuwa shambulizi hilo liliwalenga Waislamu.
Kiongozi huyo wa serikali ameongoza kikao cha usalama mapema siku ya Jumatatu na kusisitiza kuwa, Uingereza haitavumilia ugaidi na mafunzo ya kijihadi.
Ni tukio lililotokea wakati huu waumini wa dini hiyo wakiendelea kuwa katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Polisi wamesema watu wote waliojeruhiwa na aliyepoteza maisha, wote ni Waislamu.
Dereva wa basi liliwagonga Waislamu hao, amekamatwa na Polisi wanasema wanaamini alitekeza shambulizi hilo peke yake.
Uingereza hivi karibuni imeendelea kushuhudia matukio ya kigaidi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu