Masikitiko shambulizi la kigaidi London

In Kimataifa
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May anasema shambulizi la kigaidi nje ya msikiti Kaskazini mwa jiji London, linasikitisha na kuchosha.
Shambulizi hilo limesababisha kifo cha mtu mmoja na zaidi ya 10 kujeruhiwa.
Waliojeruhiwa wanaendelea kupata matibabu hospitalini.
Bi. May amesema kuwa shambulizi hilo liliwalenga Waislamu.
Kiongozi huyo wa serikali ameongoza kikao cha usalama mapema siku ya Jumatatu na kusisitiza kuwa, Uingereza haitavumilia ugaidi na mafunzo ya kijihadi.
Ni tukio lililotokea wakati huu waumini wa dini hiyo wakiendelea kuwa katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Polisi wamesema watu wote waliojeruhiwa na aliyepoteza maisha, wote ni Waislamu.
Dereva wa basi liliwagonga Waislamu hao, amekamatwa na Polisi wanasema wanaamini alitekeza shambulizi hilo peke yake.
Uingereza hivi karibuni imeendelea kushuhudia matukio ya kigaidi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu