Mawaziri sita waishio uhamishoni kuhukumiwa

   Kesi ya serikali iliyopita ya Blaise Compaoré  imeikilizwa tena  jana asubuhi May 4 katika Mahakama Kuu mjini Ogadugu.

Mawaziri sita wanaoishi uhamishoni watahukumiwa licha ya kutokuwepo.

Rais wa zamani, ambaye anachukuliwa kama waziri wa ulinzi wa zamani, ambaye alichukua uraia wa Co devowa atahukumiwa pia licha ya kutokuwepo.

Viongozi hao wa zamani wanashtumiwa “mauaji ya kukusudia na kula njama kwa kuwapiga na kuwajeruhi, kwa kukusudia waandamanaji.

Mbele ya mahakimu, mawaziri 25 wa zamani watasikilizwa kesi hiyo

Wote wanashtumiwa kwa kuwa waliamua katika kikao cha baraza la mawaziri cha Oktoba 29, 2014, kutoa wito kwa jeshi kukomesha waandamanaji waliokua wakipinga marekebisho ya Katiba.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, mawaziri walitoa wito wa kwa majeshi kuwafyatulia risasi waandamanaji, na kusababisha vifo vya watu saba na 88 kujeruhiwa.

Kwa mujibu wa chanzo cha mahakama, kesi haitadumu zaidi ya wiki mbili.

chama Compaore tayari kimeshutumu kwamba “kesi hiyo ni ya kisiasa”

Exit mobile version