Mawaziri wa nchi za Umoja wa Ulaya wamempa muongozo mpatanishi wa umoja huo anayehusika na suala la Uingereza kujitoa kutoka umoja huo Brexit, Michel Barnier.

In Kimataifa

Mawaziri wa nchi za Umoja wa Ulaya wamempa muongozo mpatanishi wa umoja huo anayehusika na suala la Uingereza kujitoa kutoka umoja huo Brexit, Michel Barnier.

Mwanadiplomasia huyo wa zamani wa Ufaransa hatarajiwi kuanzisha mazungumzo ya Brexit mpaka baada ya uchaguzi mkuu wa Uingereza mwezi ujao.

Mawaziri kutoka nchi 27 wanachama wa Umoja wa Ulaya wameridhia kanuni ambazo mpatanishi mkuu Barnier atazitumia kujadili kujitoa kwa Uingereza.

Barnier binafsi amesema hataki kufikiria kuhusu mazungumzo hayo kuvunjika na kwamba pande zote mbili huenda zikajadili mkataba wa kibiashara ikiwa masuala muhimu yanayohusiana na Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya yatakubaliwa haraka.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu