Mazungumzo ya kupunguza umaskini barani Afrika yafunguliwa Addis Ababa

In Kimataifa

Mazungumzo ya ngazi ya juu kuhusu maendeleo na kupunguza umaskini barani Afrika, na Mkutano wa jopo la washauri bingwa wa China na Afrika yamefunguliwa jana katika kituo cha mkutano cha Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia.

Waziri wa mambo ya nje wa China Bw Wang Yi na mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Afrika Bw Moussa Mahamat wamehudhuria na kuhutubia ufunguzi wa mkutano huo.

Bw Wang Yi ametoa hotuba akisema watu milioni 400 wa Afrika wanaishi katika umaskini, na Wachina zaidi ya milioni 40 wanahitaji kuondokana na umaskini hivyo Ni wajibu wa China kushirikiana katika kupambana na umaskini na kupata maendeleo ya pamoja, ambalo ni lengo la pamoja, na ni mahitaji ya maendeleo ya kijamii.

Amesema, “China inapenda kuzidisha mawasiliano na nchi za Afrika kuhusu uzoefu wa kutawala nchi, kutafuta njia ya maendeleo na kupunguza umaskini kwa kufuatana na mahitaji ya nchi za Afrika. China inapenda kubadilishana uzoefu na marafiki zetu za Afrika.”

Bw Moussa Faki Mahamat amesema anapenda ushirikiano wa pande mbili katika kupunguza umaskini upate mafanikio.

Katika mkutano huo, wataalamu na wasomi wa Afrika wameona kwamba migogoro na vita ni sababu kubwa zinazosababisha umaskini barani Afrika.

Naibu mkuu wa Chuo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Cameroon Bw Stephane Ngwanza amesema mfumo wa kisiasa wenye utulivu unafanya kazi kubwa katika kuendeleza uchumi na kuondokana na umaskini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu