Serikali imetakiwa kuweka hadharani ripoti zote mbili za madini zilizoandaliwa na kamati zilizoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza uendeshaji wa sekta ya madini nchini.
Hayo yamesemwa jijini dar es Salaam leo na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, katika mkutano na vyombo vya habari ambao ulijikita kuelezea masuala ya uchumi.
Mbowe amesema Tanzania imegeuka kituko baada Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ,kuipatia kampuni ya Acacia Ankara ya Malimbikizi ya kodi yanayozidi Sh400 trilioni.
Mbowe amesisitiza kwanza chama chake ndicho kilikuwa cha kwanza kudai mabadiliko katika sekta ya madini lakini kile kilichofanywa na serikali hakilingani na mabadiliko ambayo waliyapendekeza.
Akifafanua, amebainisha kuwa mabadiliko yaliyofanyika bungeni yamefanyika kwa papara na hayatalinufaisha taifa.
