Mbunge ataka ukomo saa za kufundishwa wanafunzi.

In Kitaifa

Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia imesisitiza kuwa
mitaala ya Elimu ya Msingi na Sekondari imeweka bayana
muda unaopaswa wanafunzi kusoma.


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda
amesema kuwa mtaala wa Elimu ya Msingi unaeleza kuwa
muda wa kusoma Elimu ya Awali na Darasa la kwanza hadi la
pili ni saa tatu (dakika 180) tu kwa siku.


Kila kipindi kimoja Waziri ameongeza, kipindi kimoja ni dakika
30.


Prof Mkenda ameongeza kuwa muda wa kusoma kwa darasa la
tatu hadi la saba ni saa sita (dakika 360) kwa siku na kila kipindi
ni dakika 40.


Kwa upande wa Elimu ya Sekondari muda wa kusoma ni saa 5
na dakika 20 na kipindi kimoja ni dakika 40.


Waziri Mkenda ametoa maelezo hayo Bungeni, Dodoma leo
Jumanne, baada ya Mbunge wa Viti Maalum Ng’wasi Kamani
kutaka kufahamu endapo Serikali imeweka katika sheria ukomo
wa saa za kufundishwa wanafunzi kama ilivyoweka kisheria
ukomo wa saa za kufanya kazi kwa waajiriwa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu