Mbunge CCM ashikiliwa kwa kuua.

In Kitaifa

Jeshi la Polisi mkoa wa Singida linamshikilia mbunge wa Manyoni, Daniel Mtuka (CCM) kwa tuhuma za kumuua mwanafunzi wa darasa la kwanza kwa kumgonga na gari alipokuwa akijaribu kuvuka barabara mkoani hapo.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida, Debora Magilingimba, Mbunge huyo  aliyekuwa akisafiri na gari lake aina ya Toyota Prado alimgonga mwanafunzi huyo na kwamba uchunguzi wa awali unaonesha kuwa chanzo cha ajali ni uzembe wake wa kutochukua tahadhari kwa watumiaji wengine wa barabara.

Kamanda Magilingimba alisema kuwa jeshi hilo linamshikilia Mtuka tangu jana kutokana na tukio hilo na watamfikisha mahakamani kwa ajili ya hatua za kisheria.

Aliongeza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Manyoni kwa uchunguzi wa madaktari.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu