Mbunge viti maalumu asema uongo asimamishwa kuhudhuria vikao vitatu.

In Kitaifa

Kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge imemsimamisha Mbunge wa Viti Maalum Conchesta Rwamlaza kuhudhuria vikao vitatu vya Bunge kuanzia Siku ya Jana kwa kosa la kusema uongo bungeni.

Akichangia Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka wa  fedha wa 2016/2017 RWAMLAZA,  amesema Mbunge wa Muleba profesa ANNA TIBAIJUKA akiwa waziri wa wizara hiyo alitumia madaraka yake vibaya kwa kujilimbikizia ardhi zaidi ya hekari 4,000.

Aidha Kamati hiyo imemsamehe Mbunge wa Arumeru Mashariki JOSHUA NASSARI ambaye mwaka jana, katika mkutano wa tatu alidharau mamlaka ya Spika na kufanya fujo baada ya Mbunge wa Chemba JUMA NKAMIA kuomba mwongozo ,akitaka kujua ni kwa nini serikali imewafukuza wanafunzi wa Diploma maalum ya Sayansi katika chuo kikuu cha Dodoma(UDOM).

Akiwasilisha maamuzi ya kamati hiyo bungeni  Mjini  Dodoma Mwenyekiti wa kamati hiyo GEORGE MKUCHIKA, amesema wabunge wote wawili walifika mbele ya kamati na kusomewa tuhuma zao na kujieleza ambapo kamati ilijiridhisha na kutoa adhabu hiyo kwa RWAMLAZA, huku ikimsamehe NASSARI baada ya kukiri na kuomba radhi.

Katika hatua nyingine bunge limepitisha azimio la makataba wa Kimataifa wa kazi za Ubaharia wa Shirika la kazi Duniani ILO wa mwaka 2016, na Azimio la Mkataba wa Kimataifa wa vitambulisho vya mabaharia namba 185 wa mwaka 2003 wa ILO.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu