Mbunge wa Dodoma Mjini, Antony Mavunde amezindua mifumo maalum ya vipimo vya kibaiolojia BIOMETRIC SYSTEM na CCTV

In Kitaifa

MBUNGE wa jimbo la Dodoma Mjini ANTHONY MAVUNDE leo  kaamezindua mifumo maalum ya vipimo vya kibaiolojia BIOMETRIC SYSTEM na CCTV Cameratika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma utakaosaidia kuboresha huduma za afya na kupunguza kero za wananchi.

Akizungumza katika uzinduzi huo MAVUNDE ambaye pia ni naibu waziri wanchi ofisi ya waziri mkuu kazi,vijana,ajira na watu wenye ulemavu amesema kama mbunge wa jimbo hilo kazi yake kubwa ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na uwepo wa mifumo hiyo utasaidia kwa kiasi kikubwa wananchi kupata huduma bora sambamba na kutambua uwajibikaji wa wafanyakazi.

Aidha itawezesha kujua watumishi wa hospitali hiyo muda wanaoingia kazini na muda wanaotoka ,ili kuwezesha kutowanyima stashiki zao hasa pale wanapotekeleza majukumu yao katika muda wa ziada.

Uzinduzi huo umehusisha CCTV Camera 4 zilizofungwa na mfumo wa Biometric mmoja vyote kwa pamoja vikiwa na gharama ya shilingi milioni 10 fedha ambazo zimetoka katika ofisi ya jimbo.

Akitoa shukrani katika uzinduzi huo Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo dokta CAROLINE  DAMIAN ,amesema tangu kufungwa kwa mfumo huo ufanisi wa kazi umeongezeka na malalamiko kutoka kwa wananchi yamepungua.

Kutokana na mafanikio hayo ameomba upatikanaji wa CCTV Camera zaidi ili kufikia idadi ya camera 100 na kuongeza idadi ya mfumo wa Biometric kuweza kufikia 3.

 

 

 

 

 

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu