Mbunge wa Mtwara Mjini (CUF), Maftaha Nachuma Akanusha Kuhamia CCM.

In Kitaifa, Siasa
Mbunge wa Mtwara Mjini (CUF), Maftaha Nachuma amewataka wananchi wa jimbo hilo kupuuza taarifa zinazosambaa kwamba ana mpango wa kujiondoa katika chama hicho.
Amesema anaendelea kuwatetea wakazi hao ili wapate maendeleo.
“CUF hawana historia ya kuhamahama vyama, hata huyo aliyeondoka ameondoka kwa masilahi binafsi. Mimi Maftaha Nachuma nitakuwa wa mwisho kuondoka CUF,” alisema jana Jumatano Desemba 6,2017.
Alisema suala la wabunge kujitoa katika nafasi zao linasababishwa na njaa kutokana na kuangalia masilahi binafsi bila kutetea wananchi.
Nachuma alisema wabunge wengi walidhani wakipata nyadhifa hizo watakuwa wananufaika kwa kupata fedha lakini sasa hilo halipo kwa kuwa ubunge siyo dili bali ni kwa ajili ya kuwatumia wananchi.
Kupitia mitandao ya kijamii imeelezwa kwamba mbunge huyo ana mpango wa kujiondoa CUF na kujiunga na CCM.
Nachuma alisema wanaosambaza taarifa hizo wana nia mbaya ya kumchafua kwa masilahi binafsi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu