Mipango ya wizi wa kura, Raila Odinga ameshutumu serikali kuwatumia wanajeshi.

In Kimataifa
Mgombea urais kupitia muungano wa upinzani nchini Kenya NASA Raila Odinga, ameishutumu serikali kuwatumia wanajeshi na maafisa wa Inteljensia kupanga wizi wa kura kuelekea Uchaguzi Mkuu mwezi Agosti.
Odinga amekishutumu chama cha Jubilee ambacho rais Uhuru Kenyatta ni mgombea wake, kuliingiza jeshi katika siasa za nchi hiyo.
Mgombea huyo ameeleza kuwa ana ushahidi kuwa wanajeshi wanapewa mafunzo katika kambi ya Embakasi jijini Nairobi na mjini Kakamega Magharibi mwa nchi hiyo kupanga namna ya kuingilia Uchaguzi huo.
Aidha, ameonya kuwa kinachotokea ni kama kile kilichojiri mwaka 2007 wakati maafisa wa usalama walipotumiwa kumsaidia Mwai Kibaki kutangazwa mshindi na kuzua machafuko yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu elfu moja.
Amewataka wanajeshi na maafisa wengine wa usalama kutoshawishika na kujiingiza kwenye siasa na badala yake kufanya kazi yao bila kuegemea upande wowote.
Hata hivyo, wanasiasa wa Jubilee wamekuwa wakikanusha madai ya Odinga na kusema hayana ukweli wowote.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu