Mipango ya wizi wa kura, Raila Odinga ameshutumu serikali kuwatumia wanajeshi.

In Kimataifa
Mgombea urais kupitia muungano wa upinzani nchini Kenya NASA Raila Odinga, ameishutumu serikali kuwatumia wanajeshi na maafisa wa Inteljensia kupanga wizi wa kura kuelekea Uchaguzi Mkuu mwezi Agosti.
Odinga amekishutumu chama cha Jubilee ambacho rais Uhuru Kenyatta ni mgombea wake, kuliingiza jeshi katika siasa za nchi hiyo.
Mgombea huyo ameeleza kuwa ana ushahidi kuwa wanajeshi wanapewa mafunzo katika kambi ya Embakasi jijini Nairobi na mjini Kakamega Magharibi mwa nchi hiyo kupanga namna ya kuingilia Uchaguzi huo.
Aidha, ameonya kuwa kinachotokea ni kama kile kilichojiri mwaka 2007 wakati maafisa wa usalama walipotumiwa kumsaidia Mwai Kibaki kutangazwa mshindi na kuzua machafuko yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu elfu moja.
Amewataka wanajeshi na maafisa wengine wa usalama kutoshawishika na kujiingiza kwenye siasa na badala yake kufanya kazi yao bila kuegemea upande wowote.
Hata hivyo, wanasiasa wa Jubilee wamekuwa wakikanusha madai ya Odinga na kusema hayana ukweli wowote.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu