Mipango ya wizi wa kura, Raila Odinga ameshutumu serikali kuwatumia wanajeshi.

In Kimataifa
Mgombea urais kupitia muungano wa upinzani nchini Kenya NASA Raila Odinga, ameishutumu serikali kuwatumia wanajeshi na maafisa wa Inteljensia kupanga wizi wa kura kuelekea Uchaguzi Mkuu mwezi Agosti.
Odinga amekishutumu chama cha Jubilee ambacho rais Uhuru Kenyatta ni mgombea wake, kuliingiza jeshi katika siasa za nchi hiyo.
Mgombea huyo ameeleza kuwa ana ushahidi kuwa wanajeshi wanapewa mafunzo katika kambi ya Embakasi jijini Nairobi na mjini Kakamega Magharibi mwa nchi hiyo kupanga namna ya kuingilia Uchaguzi huo.
Aidha, ameonya kuwa kinachotokea ni kama kile kilichojiri mwaka 2007 wakati maafisa wa usalama walipotumiwa kumsaidia Mwai Kibaki kutangazwa mshindi na kuzua machafuko yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu elfu moja.
Amewataka wanajeshi na maafisa wengine wa usalama kutoshawishika na kujiingiza kwenye siasa na badala yake kufanya kazi yao bila kuegemea upande wowote.
Hata hivyo, wanasiasa wa Jubilee wamekuwa wakikanusha madai ya Odinga na kusema hayana ukweli wowote.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu