Miradi 9 ya barabara kuzinduliwa na Rais Magufuli.

In Kitaifa
RAIS John Magufuli anatarajiwa kuzindua miradi tisa ya barabara na uwanja wa ndege ambayo itaunganisha mikoa ya Ukanda wa Kati na Magharibi nchini na nchi jirani kwa barabara za lami katika kuchochea harakati za maendeleo ya uchumi wa viwanda.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Ujenzi, Joseph Nyamhanga alisema jana kwa simu kwamba uzinduzi wa miradi hiyo utafanyika katika mikoa ya Kagera, Kigoma, Tabora na Singida kuanzia kesho hadi 25, mwaka huu.
Nyamhanga amesema ufunguzi wa Barabara ya Kigoma – Biharamulo – Lusahunga yenye urefu wa kilometa 154 utafanyika Biharamulo Mjini mkoani Kagera kesho ,huku uzinduzi wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Nyakanazi – Kibondo yenye urefu wa kilometa 50 utafanyikia Kakonko mkoani Kigoma, Julai 21.
Ameeleza kuwa uzinduzi wa Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Kidahwe –Kasulu yenye urefu wa kilometa 63 utafanyika Kasulu Mjini mkoani Kigoma, Julai 21 ambako pia ufunguzi wa barabara ya Kaliua – Kazilambwa yenye urefu wa kilometa 56 utafanyika Julai 23 Kaliua Mjini mkoani Tabora.
Aidha, Katibu Mkuu alieleza kuwa ufunguzi wa Uwanja wa Ndege wa Tabora utafanyika Julai 24 na ufunguzi wa mradi wa Manyoni – Itigi – Chanya wenye urefu wa kilometa 89.3 utafanyika Itigi mkoani Singida Julai 25, mwaka huu.
Aidha, amesema ufunguzi wa Uwanja wa Ndege wa Tabora ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuimarisha miundombinu ya viwanja vya ndege na usafiri wa anga nchini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu