Misri yaapa kukabiliana na wauaji wa watu 235 Msikitini.

In Kimataifa

Kikosi cha kijeshi cha Misri kimeanza mashambulio dhidi ya ngome za wanamgambo wanaodhaniwa ndio waliosababisha vifo vya watu wapatao 235 baada ya kuwashambulia katika eneo la rasi ya Sinai wakati walipokuwa wanatoka msikitini.

Waathiriwa wengi wa shambulio hilo lililofanywa na wanamgambo walikuwa ni wanawake, wanaume na watoto pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa wakitoka msikitini .

Serikali ya Misri imetangaza siku tatu za maombolezi kufuatia mauaji hayo.

Rais Abdel-Fattah al-Sisi ameahidi kuchukua hatua kali dhidi ya wanamgambo hao.

Eneo hilo la Sinai hukumbwa na mashambulio ya mara kwa mara yanayofanywa na wanamgambo wanaopinga serikali ya Misri, na msikiti uliolengwa ni maarufu sana na waumini wa madhehebu ya kisufi na watu wa kabila la -Sawarka wanaosemekana kuunga mkono kikamilifu serikali ya rais rais Abdel-Fattah al-Sisi .

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu