Miswada miwili ya wasilishwa kwenye kamati ya Bunge na Waziri wa Katiba na sheria.

In Kitaifa
Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi, amewasilisha kwenye Kamati Maalumu ya Bunge miswada miwili, huku akisisitiza wajumbe kujadili kwa manufaa ya taifa na si maslahi binafsi.
Miswada iliyowasilishwa jana ni Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba ya Maliasili za Nchi, na ule wa Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusu Umiliki wa Maliasili wa Mwaka 2017.
Aidha, kamati leo zitaanza kukutana na wadau wa madini ili kukusanya maoni kabla ya muswada huo kujadiliwa na bunge katika vikao.
Akiwasilisha muswada wa pili wa Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba ya Maliasili za Nchi, Profesa Kabudi amesema mikataba hiyo haiendi kinyume na Katiba na ya misingi ya sheria za kimataifa kwa sababu Tanzania ni sehemu ya dunia.
Kabudi amesema kwa mujibu wa masharti yaliyopendekezwa baada ya kubaini kuna masharti hasi katika mikataba hiyo, Bunge linaweza kuitaka serikali kufanya majadiliano upya na upande wa pili wa mkataba ili kuondoa masharti hayo.
Aidha, Muswada huo unakusudia kutekeleza masharti ya Ibara ya 27 ya Katiba, ambayo pamoja na mambo mengine, inamtaka kila Mtanzania kulinda na kusimamia kikamilifu rasilimali za nchi kwa maslahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu