Mkutano wa wagombea urais na IEBC Kenya waahirishwa.

In Kimataifa

Tume ya Uchaguzi Kenya imeahirisha mkutano ambao ulikuwa umepangwa kufanyika leo, kati ya mwenyekiti wa tume hiyo na wagombea wa urais.

Mkutano huo ulikuwa umepangiwa kufanyika saa nane na nusu adhuhuri, lakini tume hiyo imetoa taarifa na kusema umeahirishwa.

Uchaguzi mpya wa marudio nchini Kenya umepangiwa kufanyika siku ya Alhamisi wiki ijayo tarehe 26 mwezi huu.

Ingawa Rais Uhuru Kenyatta amesisitiza yuko tayari kwa uchaguzi huo na utaendelea, mgombea wa upinzani Raila Odinga alijiondoa wiki iliyopita.

Jana Bw Raila Odinga ambaye ni mgombea wa muungano wa National Super Alliance Nasa, alitangaza siku hiyo badala ya kushiriki uchaguzi, wafuasi wake watafanya maandamano makubwa kote nchini humo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu