Mkuu wa Benki ya Gambia afutwa kazi.

In Kimataifa
  Mkuu wa Benki Kuu ya Gambia aliyekuwa akihudumu wakati wa utawala wa Yahya Jammeh, Amadou Colley, amefutwa kazi.
Hakuna sababu zozote zilizotolewa kuhusiana na kufutwa kwake.
Bw Colley mwenyewe ameambia Reuters kwamba hajui ni kwa nini ameachishwa kazi.
Bw Colley alihudumu chini ya Rais Jammed ambaye alituhumiwa na baadhi ya maafisa wa serikali mpya kwamba alipora mamilioni ya dola kutoka kwa hazina ya serikali wakati wa utawala wake wa miaka 22.
Tangu achukue madaraka Januari, Rais Adama barrow amekuwa akiwafuta kazi na kuteua maafisa wapya katika nyadhifa zenye ushawishi serikalini.
Bw Barrow alimshinda Jamme kwenye uchaguzi mkuu Desemba, ingawa rais huyo alikubali kuondoka wiki kadha baadaye baada ya kushinikizwa na jamii ya kimataifa.
Kwa sasa, Jammeh anaishi uhamishoni Equatorial Guinea

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu