Mkuu wa Jeshi la Polisi afungua majengo mawili.

In Kitaifa
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro amefungua majengo mawili ya ofisi ya usalama barabarani  huku akiwahimiza askari wa jeshi hilo Mkoa wa Kipolisi wa Tarime/Rorya kufanya kazi kwa weledi, uwaadilifu, kujituma na kuwa na mahusiano na kushirikiana na wananchi katika ulinzi wa taifa na kupambana na uhalifu.
Akizungumza na askari hao wa Polisi wa Tarime/ Rorya  katika hafla ya uzinduzi wa majengo hayo yaliyojengwa kwa gharama zaidi ya Sh milioni 40 sirro amewataka askari polisi kufanya kazi kwa kufuata sheria bila kumuonea mtu.
Kamanda wa Polisi wa Tarime/ Rorya, Henry Mwaibambe amesema majengo hayo yamegharimu milioni 21 laki tisa na sabini na nane elfu, wakati jengo la michezo ambalo halijakamilika linatarajiwa kukamilika kwa zaidi ya Sh milioni 25.
Aidha amezitaja changamoto nyingine zinazokabili Kikosi cha Usalama Barabarani ni magari, pikipiki za kufanya doria ili kudhibiti vitendo vya makosa ya barabarani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu