Mkuu wa Jeshi la Polisi afungua majengo mawili.

In Kitaifa
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro amefungua majengo mawili ya ofisi ya usalama barabarani  huku akiwahimiza askari wa jeshi hilo Mkoa wa Kipolisi wa Tarime/Rorya kufanya kazi kwa weledi, uwaadilifu, kujituma na kuwa na mahusiano na kushirikiana na wananchi katika ulinzi wa taifa na kupambana na uhalifu.
Akizungumza na askari hao wa Polisi wa Tarime/ Rorya  katika hafla ya uzinduzi wa majengo hayo yaliyojengwa kwa gharama zaidi ya Sh milioni 40 sirro amewataka askari polisi kufanya kazi kwa kufuata sheria bila kumuonea mtu.
Kamanda wa Polisi wa Tarime/ Rorya, Henry Mwaibambe amesema majengo hayo yamegharimu milioni 21 laki tisa na sabini na nane elfu, wakati jengo la michezo ambalo halijakamilika linatarajiwa kukamilika kwa zaidi ya Sh milioni 25.
Aidha amezitaja changamoto nyingine zinazokabili Kikosi cha Usalama Barabarani ni magari, pikipiki za kufanya doria ili kudhibiti vitendo vya makosa ya barabarani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu