Mkuu wa mashtaka nchini Sweden ameamua kuachana na mashtaka ya ubakaji dhidi ya mwanzilishi wa mtandao wa uchunguzi wa Wikileaks, Julian Assange.

In Kimataifa

Mkuu wa mashtaka nchini Sweden ameamua kuachana na mashtaka ya ubakaji dhidi ya mwanzilishi wa mtandao wa uchunguzi wa Wikileaks, Julian Assange.

Marianne Ny amesema amefikia uamuzi kwa sababu ameshindwa kumpa Assange taarifa ya maandishi kuhusu mashtaka yanayomkabili.Assange mwenye umri wa maika 45, amekuwa akiishi katika Ubalozi wa Ecuador jijini London kuanzia mwaka 2012.

Wakili wake, Per Samuelson, amesema uamuzi huo wa kiongozi wa mashtaka ni ushindi mkubwa kwa Assange.

Raia huyo wa Australia amekuwa akisema hawezi kwenda nchini Sweden kwa sababu ana hofu kuwa atasafirishwa kwa nguvu kwenda nchini Marekani, anakotuhumiwa kuvujisha siri za serikali.

Hata hivyo, Polisi jijini London wanasema watamkamata Assange ikiwa ataondoka katika Ubalozi huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu