Waziri wa Ujenzi Atoa siku saba kwa kampuni ya reli Tanzania TRL kukarabati daraja la reli la Ruvu.

In Kitaifa

Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Professa Makame Mbarawa ametoa siku saba kwa Kampuni ya Reli Tanzania TRL, kukamilisha ukarabati wa daraja la Reli la Ruvu lililoharibiwa na kukatika hivi karibuni kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini na kusababisha huduma za usafirishaji abiria na mizigo kusimama.

Waziri Mbarawa amesema hayo jana alipotembelea daraja hilo kwa lengo la kukagua na kuona maendeleo ya Ujenzi wa daraja la Ruvu ambao umekwisha anza na kusisitiza kuharakishwa ukamilikaji wa ujenzi huo ili kuruhusu huduma mbalimbali za usafirishaji kutoka ndani na nje ya nchi ambazo zimekwama kwa muda.

Aidha Waziri Profesa Mbarawa amesema kwa sasa Serikali ina mpango wa kudumu wa kuhakikisha madaraja yote ya reli nchini yanafanyiwa ukarabati wa kudumu ili kuhakikisha changamoto na athari za uharibifu wa miundombinu ya reli unaotokana na athari za mvua hazijitokezi tena huku akitaja mchakato uliopo sasa wa uanzishwaji wa Reli ya kisasa ambao utachangia kwa kiasi kikubwa kuondosha matatizo ya uharibifu wa madaraja ya Reli.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Reli Tanzania TRL na Kampuni Hodhi ya Miundombinu na Rasilimali za Reli Masanja Kadogosa amesema Kampuni hiyo itatekeleza agizo hilo la Waziri Mbarawa kwa wakati kutokana na usafiri huo wa reli kuwa tegemeo la wananchi wengi , huku akitaja gharama zitakazotumika katika ujenzi wa Daraja hilo kuwa ni shilingi milioni 328 za kitanzania.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu