Mkuu wa Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Festo Kiswaga amewataka watendaji wa Halmashauri ya Bariadi Mjini na Vijijini kuhakikisha fedha zote za makusanyo ya ndani zinazokusanywa na kikosi kazi zinaingizwa kwenye akaunti sahihi kabla ya kufanyiwa matumizi ya aina yoyote ili kudhibiti matumizi yasiyorasmi na unadhirifu wa fedha za umma.

In Kitaifa

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Festo Kiswaga amewataka watendaji wa Halmashauri ya Bariadi Mjini na Vijijini kuhakikisha fedha zote za makusanyo ya ndani zinazokusanywa na kikosi kazi zinaingizwa kwenye akaunti sahihi kabla ya kufanyiwa matumizi ya aina yoyote ili kudhibiti matumizi yasiyorasmi na unadhirifu wa fedha za umma.

Mkuu huyo wa Wilaya alitoa agizo hilo katika kikao cha Baraza la madiwani kilichofanyika mjini Bariadi, ambapo amesema Serikali wilayani humo kupitia kamati ya ulinzi na usalama ilibani kusua sua kwa ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri hizo, hivyo kushauri kuundwa kikosi kazi ili kukusanya mapato ya ndani na jambo ambalo limeleta faida na kufikia lengo la makusanyo katika mwaka 2017.

Katika hatua nyingine Kiswaga amewataka wanunuzi wote wa zao la pamba kuhakikisha wanalipa madeni yao yote ya ushuru wa pamba katika Halmashauri hizo, kwani vinginevyo hawataruhusiwa kununua wala kupatiwa leseni za kununua pamba wilayani Bariadi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu