Mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola umetangazwa Kaskazini Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

In Kimataifa
Mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola umetangazwa Kaskazini Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Shirika la afya duniani WHO limethibitisha kutokea kwa mlipuko huo ambao umesababisha vifo vya watu watatu tangu mwaka tarehe 22 mwezi Aprili mwaka huu.
Eneo la msitu wa Equitorial katika mkoa wa Bas-Uele mpakani na Jamhuri ya Afrika ya Kati ndilo lililoathiriwa.
Waziri wa afya nchini humo Oly Ilunga amethibitisha uwepo wa ugonjwa huo lakini akatoa wito kwa wananchi kutokuwa na wasiwasi.
WHO inasema inashirikiana kwa karibu na serikali ya DRC kuhakikisha kuwa wanafanikiwa kudhibiti ugonjwa huo.
Mara ya mwisho kwa Ebola kulikumba taifa hilo, ilikuwa ni mwaka 2014 na kusababisha watu 49 kupoteza maisha lakini baadaye maafisa wa afya wakafanikiwa kuudhibiti.
Ugonjwa huu ulisumbua sana Mataifa ya Magharibi mwaka 2013 na kusababisha vifo vya watu 11,300 na kuwambukiza wengine nchini Guinea, Sierra Leone na Liberia.
Hata hivyo, baadhi ya wanajeshi walijitokeza baadaye na kudai kuwa hawakushauriwa kuhusu hatua iliyofikiwa na msemaji wao.
Rais Outtara amekuwa akisema kuwa nchi yake inapitia kipindi kigumu cha kisiasa kwa sababu ya kushuka kwa biashara ya Cocoa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu