Mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola umetangazwa Kaskazini Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

In Kimataifa
Mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola umetangazwa Kaskazini Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Shirika la afya duniani WHO limethibitisha kutokea kwa mlipuko huo ambao umesababisha vifo vya watu watatu tangu mwaka tarehe 22 mwezi Aprili mwaka huu.
Eneo la msitu wa Equitorial katika mkoa wa Bas-Uele mpakani na Jamhuri ya Afrika ya Kati ndilo lililoathiriwa.
Waziri wa afya nchini humo Oly Ilunga amethibitisha uwepo wa ugonjwa huo lakini akatoa wito kwa wananchi kutokuwa na wasiwasi.
WHO inasema inashirikiana kwa karibu na serikali ya DRC kuhakikisha kuwa wanafanikiwa kudhibiti ugonjwa huo.
Mara ya mwisho kwa Ebola kulikumba taifa hilo, ilikuwa ni mwaka 2014 na kusababisha watu 49 kupoteza maisha lakini baadaye maafisa wa afya wakafanikiwa kuudhibiti.
Ugonjwa huu ulisumbua sana Mataifa ya Magharibi mwaka 2013 na kusababisha vifo vya watu 11,300 na kuwambukiza wengine nchini Guinea, Sierra Leone na Liberia.
Hata hivyo, baadhi ya wanajeshi walijitokeza baadaye na kudai kuwa hawakushauriwa kuhusu hatua iliyofikiwa na msemaji wao.
Rais Outtara amekuwa akisema kuwa nchi yake inapitia kipindi kigumu cha kisiasa kwa sababu ya kushuka kwa biashara ya Cocoa.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu