Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani Mwanza na aliyewahi kuwa mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexanda Mnyeti, amefikishwa katika mahakama kuu kanda ya manyara kwa matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishaia hasara ya zaidi ya shilingi bili 1 kampuni ya uwindaji ya HSK Safari Limited iliyopo Simanjiro Mkoani Manyara.
Mnyeti anadaiwa kushirikiana na afisa mendaji wa kata ya Emboreti Wilayani Simanjiro Nasalee Salum,kunyang’anya kitalu cha uwindaji cha kampuni ya HSK Safari Limited bila kufuata sheria.