Wafanyabiashara na wakulima wametakiwa kutumia fursa zinazojitokeza ikiwa ni pamoja na kuhudhuria kwenye maonyesho mbalimblai yanayojitokeza ili kuweza kulata taarifa safii ya namna gani ya kufanya Kilimo biashara
Wito huo umetolewa na Mkuu wa mkoa wa Arusha Mh John Mongela wakati Akifungua maonyesho ya chakula na kilimo Tanzfood yanayoendelea katika viwanja vya magereza Kisongo jijini.
Kwa upande wake mwandaaaji wa maonyesho hayo Dominic Shoo Amesema kuwa maonyesho hayo ni mara ya kwanza kufanyika ikiwa lengo ni kuweza kuwakutanisha wafanyabiashara na wakulima na kujengeana uwezo
Kwa upande wao wadau mbalimbali waliohudhuria kwenye maonyesho hayo wamesema yatawanufaisha hasa katika kuwakutanisha na mataifa mbalimbali na kujengeana uwezo kwenye biashara zao,,
Maonyesho hayo yamefungulia leo na yanatarajiwa kufungwa siku ya jumapili