Mpango na maelekezo ya miaka miwili kuidhinishwa baada ya Uingereza kujitoa kwenye jumuia ya umoja wa ulaya.

In Kimataifa
Wakuu wa nchi kutoka jumuiya ya umoja wa Ulaya wanatarajia kuonesha mshikamano wao wakati wa mkutano wao Jumamosi hii ambapo wataidhinisha mpango wa maelekezo ya miaka miwili kwa nchi ya Uingereza kujitoa kwenye umoja huo.
Wakuu hao kutoka nchi 27 zilizosalia wanatarajiwa kuitaka Uingereza kutatua masuala muhimu kuhusu kujitoa kwake kunakohusu watu, fedha na Jamhuri ya Ireland kabla ya kufanyika kwa mazungumzo yoyote ya baadae.
Mkutano huu unafanyika huku joto la kujitoa kwa Uingereza likiwa linapanda pamoja na vita ya meneno kati ya kansela wa Ujerumani Angela Merkel na waziri mkuu wa Uingereza Theresa May kuhusu majadiliano.
Viongozi hao pia wanatarajia kuunga mkono wazo wa nchi ya Ireland Kaskazini kuwa mwanachama wa umoja huo ikiwa itaungana na Ireland na kuitaka Uhispania kuwa na usemi kuhusu athari za eneo la Gibraltar.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu