Mpigapicha ashinda kesi kuhusu selfie ya tumbili.

In Kimataifa

Mpiga picha mmoja ameshinda kesi iliyodumu kwa miaka miwili, dhidi ya kundi la kutetea haki za wanyama kuhusu haki za kumiliki picha ambayo ilipigwa na tumbili.

Tumbili kwa jina Naruto alidaiwa kujipiga picha hiyo katika msimu mmoja Indonesia mwaka 2011, alipoichukua kamera iliyokuwa inamilikiwa na David Slater kutoka Monmouthshire.

Majaji nchini Marekani wamesema kuwa,tumbili huyo hangekabidhiwa haki miliki ya picha hiyo.

Watetezi wa haki za wanyama kutoka kwa kundi la People for the Ethical Treatment of Animals (Peta), ambao walikuwa wamewasilisha kesi hiyo kwa niaba ya tumbili huyo, walisema mnyama huyo anafaa kufaidi kwa njia fulani.

Kesi hiyo ya Peta “kwa niaba ya tumbili” imetupiliwa mbali lakini Bw Slater amekubali kutoa asilimia 25 ya mapato yatakayotokana na picha hiyo siku zijazo.

Bwana Slater alidai kuwa ilimchukua siku tatu kuruhusiwa kuwakaribia tumbili hao.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu