Mrisho Gambo awataka waajiri wa wafanyakazi katika sekta binafsi kufuata maelekezo ya Serikali.

In Kitaifa

Mkuu wa mkoa wa  Arusha   Mrisho Gambo amewataka  waajiri wa
wafanyakazi katika sekta  binafsi kufata maelekezo ya serikali
kuhakikisha watumishi wote kima chao  cha chini kinaanzia shs laki
tatu na nusu kama ambavyo serikali imesema.

Gambo ameyasema hayo  jijini  Arusha katika viwanja wa Sheikh
Amri Abed ,wakati wa maazimisho ya siku ya wafanyakazi  na kusema changamoto kubwa imewalenga wafanyakazi wa sekta
binafsi  ,ambao mishahara yao kima cha chini ni shilingi  laki moja tofauti na
maelekezo ya serikali ambapo kima cha china kinaanzia laki tatu na
nusu.
Aidha Gambo amesema ni kosa kwa mtumishi yoyote kufanyishwa kazi na mtu
yoyote au kampuni yoyote, bila kuwa na mikataba ya ajira hivyo
watumishi wa idara ya kazi mkoa wa Arusha wametakiwa kuhakikisha
wanapitia waajiri wote wa serikali na sekta binfsi, kuhakikisha kwamba
wanawapatia mikataba ya ajira watumishi wao na wale waajiri wote na
ambao hawatafanya hivyo watachukuliwa hatua za kisheria.

Kuhusu kutokupanda kwa mishahara  Gambo amesema changamoto hiyo
imesababishwa na wafanyakazi waliokua wanatumia vyeti visivyokuwa
sahihi  na wafanyakazi hewa, na amewahakikishia watumishi wote wa mkoa
wa Arusha kuwa  watumishi wote wanaostahili kupanda daraja
watapandishwa daraja na wanaodai maslahi  yao , watapewa baada ya
kukamilika kwa zoezi la kuwabaini wafanyakazi hewa na wasio kuwa na
vyeti halali.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu