Mrithi wa Kabila kupatikana Desemba 2018.

In Kimataifa, Siasa

Hatimaye Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo CENI, imetangaza kwamba uchaguzi mkuu wa rais unaosubiriwa sana utafanyika Desemba 23 2018 na siyo Aprili 2019 kama ilivyotangazwa awali.
Tarehe hiyo imetangazwa baada ya ukosoaji mkubwa kwamba Rais Joseph Kabila, amekuwa akiahirisha uchaguzi mara kwa mara ili abaki anang’ang’ania madaraka.
CENI imetangaza tarehe hiyo siku chache baada ya balozi wa Marekani kwenye Umoja wa Mataifa Nikki Haley, kuonya uwezekano wa kuzuka vurugu ikiwa uchaguzi huo hautafayika haraka.
Hata hivyo, upinzani umesema haukubaliani na tarehe hiyo huku ukimtaka Rais Kabila kuondoka madarakani.
Uchaguzi mkuu ulipaswa kufanyika Desemba 2016 baada ya mihula miwili ya uongozi wa Kabila kumalizika, lakini umekuwa ukiahirishwa na alikataa kujiuzulu hali iliyoibua mgogoro wa kisiasa katika nchi hiyo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu