Msanii wa Kenya, Jaguar akana shitaka la kuua vijana Wawili

Mwanamuziki Mashuhuri Nchini Kenya, Charles Njagua Kanyi anayejulikana Kisanii kwa jina la Jaguar amekana shitaka la kusababisha Vifo vya vijana wawili waendesha bodaboda kufuatia ajali iliyosababishwa na gari lake aina ya Range Rover Spot.

Katika ajali hiyo iliyotokea march 21 mwaka huu katika barabara ya sagana Makutano, ilisababisha Vifo vya watu wawili ambapo alikuwa mwendesha bodaboda na abiria wake.

Gari la Jaguar likiwa katika eneo la ajali hiyo

Akijibu Shtaka hilo jana Jumanne ya tarehe 11 katika mahakama ya Baricho iliyopo eneo la Kirinyaga, Pamoja na uchunguzi kuendelea kufanyika Jaguar alikana shtaka hilo akiwa na ujasiri wa kutosha tofauti na wiki tatu zilizopita ambapo pia alisomewa shitaka hilo na kuonekana kama mtu mwenye wasiwasi na mawazo muda wote akiwa mahakamani.

Jaguar ambaye anagombea Ubunge katika eneo bunge la Starehe ameonekana kupata upinzani mkubwa kutoka kwa wananchi wakisema kwamba amejiharibia kwa tukio hilo japokuwa yeye bado anaamini kwamba katika uchaguzi huo wa mwaka huu ataibuka Kidedea na kuingia Bungeni.

Kwa upande wa familia za waliopoteza maisha zinataka haki itendeke kwa usawa bila kuangalia jina la Jaguar na heshima aliyonayo katika Nchi ya Kenya.

Hata hivyo Jaguar aliachiwa kwa dhamana ya sh. 50,000 za kenya sawa na  shilingi 120,000 ya Tanzania  huku kesi hiyo ikiahirishwa hadi tarehe 8 June mwaka huu ambapo itakuwa ni miezi  miwili kabla ya uchaguzi.

Exit mobile version