Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric ameitaka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kubainisha tarehe za uchaguzi wa kitaifa

In Kimataifa
Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric ameitaka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kubainisha tarehe za uchaguzi wa kitaifa, baada ya uchaguzi uliotarajiwa kufanyika Desemba kuahirishwa kwa sababu za usalama.
Rais Joseph Kabila, ambaye amekuwa uongozini tangu 2001, alikataa kuachia madaraka baada ya kumalizika muhula wake wa pili Desemba mwaka jana, hatua iliyozusha maandamano yenye machafuko ambayo yamewaacha maelfu ya watu bila makazi katika mkoa wa Kasai.
Tangazo la jana, ambalo lilitolewa na kiongozi wa tume ya uchaguzi ya Congo – CENI, linakwenda kinyume na makubaliano ya kipindi cha mpito yaliyosimamiwa na Kanisa Katoliki mwishoni mwa mwaka jana kumzuia Kabila kugombea kwa muhula wa tatu.
Katika mahojiano yaliyochapishwa mwezi uliopita na gazeti la Ujerumani la Der Spiegel, Kabila amesema “hakuwa ameahidi chochote” katika makubaliano hayo ya Desemba.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu