Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric ameitaka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kubainisha tarehe za uchaguzi wa kitaifa

In Kimataifa
Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric ameitaka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kubainisha tarehe za uchaguzi wa kitaifa, baada ya uchaguzi uliotarajiwa kufanyika Desemba kuahirishwa kwa sababu za usalama.
Rais Joseph Kabila, ambaye amekuwa uongozini tangu 2001, alikataa kuachia madaraka baada ya kumalizika muhula wake wa pili Desemba mwaka jana, hatua iliyozusha maandamano yenye machafuko ambayo yamewaacha maelfu ya watu bila makazi katika mkoa wa Kasai.
Tangazo la jana, ambalo lilitolewa na kiongozi wa tume ya uchaguzi ya Congo – CENI, linakwenda kinyume na makubaliano ya kipindi cha mpito yaliyosimamiwa na Kanisa Katoliki mwishoni mwa mwaka jana kumzuia Kabila kugombea kwa muhula wa tatu.
Katika mahojiano yaliyochapishwa mwezi uliopita na gazeti la Ujerumani la Der Spiegel, Kabila amesema “hakuwa ameahidi chochote” katika makubaliano hayo ya Desemba.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu