Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric ameitaka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kubainisha tarehe za uchaguzi wa kitaifa

In Kimataifa
Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric ameitaka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kubainisha tarehe za uchaguzi wa kitaifa, baada ya uchaguzi uliotarajiwa kufanyika Desemba kuahirishwa kwa sababu za usalama.
Rais Joseph Kabila, ambaye amekuwa uongozini tangu 2001, alikataa kuachia madaraka baada ya kumalizika muhula wake wa pili Desemba mwaka jana, hatua iliyozusha maandamano yenye machafuko ambayo yamewaacha maelfu ya watu bila makazi katika mkoa wa Kasai.
Tangazo la jana, ambalo lilitolewa na kiongozi wa tume ya uchaguzi ya Congo – CENI, linakwenda kinyume na makubaliano ya kipindi cha mpito yaliyosimamiwa na Kanisa Katoliki mwishoni mwa mwaka jana kumzuia Kabila kugombea kwa muhula wa tatu.
Katika mahojiano yaliyochapishwa mwezi uliopita na gazeti la Ujerumani la Der Spiegel, Kabila amesema “hakuwa ameahidi chochote” katika makubaliano hayo ya Desemba.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu