Mshauri wa maswala ya usalama Michael Flynn Kuhojiwa na aliyekua mkuu wa upelelezi kawaandikia barua maafisa na rafiki zake.

In Kimataifa
     Maseneta wanaochunguza uhusiano uliopo kati ya Rais Donald Trump na Urusi wamemwagiza aliyekuwa mshauri wa maswala ya usalama nchini Michael Flynn afike mbele yao kuhojiwa. Wanataka atoe stakabadhi alizo nazo. Bwana Flynn alikataa kufanya hivyo majuma mawili yaliyopita.
Alilazimishwa kujiuzulu mnamo Februari baada ya kusema uongo juu ya mawasiliano yake ya simu na balozi wa Urusi nchini humo.
Wakati huo huo;
Aliyekuwa mkuu wa idara ya upelelezi nchini Marekani, James Comey, aliyetimuliwa kazini Jumanne, amejibu hatua hiyo kwa kuwaandikia barua maafisa katika idara hiyo na rafiki zake. Alisema hatapoteza wakati wake juu ya hatua iliyochukuliwa au jinsi ilivyotekelezwa na akasema kuwa kwa muda mrefu ameamini kuwa Rais ana kila sababu ya kumtimua kazini mkurugenzi wa FBI kwa sababau moja au hata bila sababu yo yote.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu