Mshauri wa maswala ya usalama Michael Flynn Kuhojiwa na aliyekua mkuu wa upelelezi kawaandikia barua maafisa na rafiki zake.

In Kimataifa
     Maseneta wanaochunguza uhusiano uliopo kati ya Rais Donald Trump na Urusi wamemwagiza aliyekuwa mshauri wa maswala ya usalama nchini Michael Flynn afike mbele yao kuhojiwa. Wanataka atoe stakabadhi alizo nazo. Bwana Flynn alikataa kufanya hivyo majuma mawili yaliyopita.
Alilazimishwa kujiuzulu mnamo Februari baada ya kusema uongo juu ya mawasiliano yake ya simu na balozi wa Urusi nchini humo.
Wakati huo huo;
Aliyekuwa mkuu wa idara ya upelelezi nchini Marekani, James Comey, aliyetimuliwa kazini Jumanne, amejibu hatua hiyo kwa kuwaandikia barua maafisa katika idara hiyo na rafiki zake. Alisema hatapoteza wakati wake juu ya hatua iliyochukuliwa au jinsi ilivyotekelezwa na akasema kuwa kwa muda mrefu ameamini kuwa Rais ana kila sababu ya kumtimua kazini mkurugenzi wa FBI kwa sababau moja au hata bila sababu yo yote.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu