Mshukiwa mmoja ametambuliwa katika tukio la mlipuko uliotokea katika lango la shule ya chekechea mashariki mwa China wakati idadi ya vifo ikipanda hadi watu wanane.

In Kimataifa

Mshukiwa mmoja ametambuliwa katika tukio la mlipuko uliotokea katika lango la shule ya chekechea mashariki mwa China wakati idadi ya vifo ikipanda hadi watu wanane.

Mlipuko huo ulitokea wakati jamaa za wanafunzi walikuwa wanawachukua kutoka shuleni watoto wao jana jioni.

Shirika la habari la Xinhua limesema polisi inachunguza mlipuko huo kama tukio la uhalifu na ikasema imemlenga mshukiwa mmoja ambaye haikutoa maelezo zaidi kumhusu.

Haijabainika kama mshukiwa huyo alikamatwa na hakuna ripoti iliyotolewa kuhusu lengo la mlipuko huo.

Aliyeshuhudia amenukuliwa na chombo cha habari akisema kulikuwa mtungi wa gesi uliokuwa kwenye duka moja la chakula kandoni mwa barabara ndio ulisababisha mlipuko huo.

Zaidi ya watu 65 walijeruhiwa na wanane kati yao wako katika hali mahututi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu