Mshukiwa mmoja ametambuliwa katika tukio la mlipuko uliotokea katika lango la shule ya chekechea mashariki mwa China wakati idadi ya vifo ikipanda hadi watu wanane.

In Kimataifa

Mshukiwa mmoja ametambuliwa katika tukio la mlipuko uliotokea katika lango la shule ya chekechea mashariki mwa China wakati idadi ya vifo ikipanda hadi watu wanane.

Mlipuko huo ulitokea wakati jamaa za wanafunzi walikuwa wanawachukua kutoka shuleni watoto wao jana jioni.

Shirika la habari la Xinhua limesema polisi inachunguza mlipuko huo kama tukio la uhalifu na ikasema imemlenga mshukiwa mmoja ambaye haikutoa maelezo zaidi kumhusu.

Haijabainika kama mshukiwa huyo alikamatwa na hakuna ripoti iliyotolewa kuhusu lengo la mlipuko huo.

Aliyeshuhudia amenukuliwa na chombo cha habari akisema kulikuwa mtungi wa gesi uliokuwa kwenye duka moja la chakula kandoni mwa barabara ndio ulisababisha mlipuko huo.

Zaidi ya watu 65 walijeruhiwa na wanane kati yao wako katika hali mahututi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu