Mshukiwa mmoja ametambuliwa katika tukio la mlipuko uliotokea katika lango la shule ya chekechea mashariki mwa China wakati idadi ya vifo ikipanda hadi watu wanane.

In Kimataifa

Mshukiwa mmoja ametambuliwa katika tukio la mlipuko uliotokea katika lango la shule ya chekechea mashariki mwa China wakati idadi ya vifo ikipanda hadi watu wanane.

Mlipuko huo ulitokea wakati jamaa za wanafunzi walikuwa wanawachukua kutoka shuleni watoto wao jana jioni.

Shirika la habari la Xinhua limesema polisi inachunguza mlipuko huo kama tukio la uhalifu na ikasema imemlenga mshukiwa mmoja ambaye haikutoa maelezo zaidi kumhusu.

Haijabainika kama mshukiwa huyo alikamatwa na hakuna ripoti iliyotolewa kuhusu lengo la mlipuko huo.

Aliyeshuhudia amenukuliwa na chombo cha habari akisema kulikuwa mtungi wa gesi uliokuwa kwenye duka moja la chakula kandoni mwa barabara ndio ulisababisha mlipuko huo.

Zaidi ya watu 65 walijeruhiwa na wanane kati yao wako katika hali mahututi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu