Mtaalamu mmoja wa uwindaji ameuwawa baada ya kulaliwa na ndovu ambaye alikuwa amepigwa risasi

Mtaalamu mmoja wa uwindaji ameuwawa baada ya kulaliwa na ndovu ambaye alikuwa amepigwa risasi

anaripotiwa kupigwa risasi wakati alimuinua Theunis Botha akitumia pembe yake kabla ya kuanguka na kufariki huku akimlalia na kumuaa bwana Botha.

Amekuwa akiongoza kundi la wawindaji karibu na mbuga ya Hwange nchini Zimbabwe wakati alifariki.

Mbuga hiyi ndiko simba Cecil aliuwawa na muwindaji mmarekani mwezi Julai mwaka 2015 na kuzua shutuma kote duniani. Bwana Botha ana umri wa miaka 51 na baba wa watoto watano kutoka mkoa wa Limpopo nchini Afrika Kusini.

Mtandao wa Botha unasema kuwa alikuwa na ujuzi wa kuwinda Simba na Chui.

Vyombo vya habari nchini Afrika Kusini vilisema kuwa bwana Botha alikuwa rafiki wa muwindaji mwingine Van Zyl, ambaye mabaki yake yalipatikana ndani ya mamba mwezi uliopita.

 

 

 

Exit mobile version