Mufti wa Tanzania awataka watanzania na waislamu wote kulinda amani ya Nchi.

In Kitaifa

MUFTI wa Tanzania na Shekhe Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeiry Bin Ally amehimiza umoja, upendo na mshikamano kwa Waislamu na Watanzania kwa ujumla na pia amewataka kulinda Amani ya nchi.

Pia, amesema Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata) lina mipango mikubwa ya kuinua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Hali kadhalika, Mufti ameomba viongozi wa dini nchini, kufanya dua ndogo na kubwa katika kuliombea taifa na Rais Dk John Magufuli kwa moyo wa uzalendo katika kuleta maendeleo bila kujali itikadi za dini, siasa na ukabila.

Amesema hayo kwenye Baraza la Idd, lililofanyika kitaifa kwenye msikiti wa Masjid Riadha, mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro mara baada ya kuswali sala ya Idd.

Kuhusu maboresho ya uongozi wa Bakwata, Mufti amesema baraza limekuwa imara zaidi kwa kushirikisha taasisi zote za Kiislamu, jambo ambalo linaepusha misuguano isiyo na tija mara kwa mara.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na Wajumbe wa Baraza la Ulamaa, Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof Jumanne Maghembe, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira, IGP mstaafu, Said Mwema, Mbunge wa Moshi Mjini, Jaffary Michael, wakuu wa wilaya za mkoa hwa Kilimanjaro na viongozi mbalimbali wa dini na serikali.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu