Wengi walitarajia kwamba Rais Robert Mugabe angetumia hotuba yake ya moja kwa moja kwenye runinga kujiuzulu, hasa baada ya kuvuliwa uongozi wa chama cha Zanu-PF.
Lakini hilo halijafanyika.
Badala yake amesema ni yeye atakayeongoza mkutano mkuu wa chama hicho wiki chache zijazo.
Amewahimiza raia wa Zimbabwe kuvumiliana na kusameheana.
