Mugabe ahutubia Taifa bila kujiuzulu.

Wengi walitarajia kwamba Rais Robert Mugabe angetumia hotuba yake ya moja kwa moja kwenye runinga kujiuzulu, hasa baada ya kuvuliwa uongozi wa chama cha Zanu-PF.

Lakini hilo halijafanyika.

Badala yake amesema ni yeye atakayeongoza mkutano mkuu wa chama hicho wiki chache zijazo.

Amewahimiza raia wa Zimbabwe kuvumiliana na kusameheana.

Exit mobile version