Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani saa chache baada ya jeshi la Zimbabwe kutwaa madaraka, kwa mujibu wa mtandao maarufu wa habari nchini Afrika Kusini.

“Mugabe anajiandaa kuondoka madarakani,” mtandao wa wa News24 uliandika bila ya kutoa taarifa zaidi.

Misukusuko ya kisiasa imekuwa ikiongezeka tangu Mugabe hivi majuzi amfute Emmerson Mnangagwa, mshirika wake wa miaka mingi kama makamu wa Rais.

Exit mobile version