Mugabe: Mnangawa aliwauliza waganga ni lini nitakufa.

Rais wa Zimbabwe Robert Kugabe amemlaumu makamu wake wa rais aliyefutwa, Emmerson Mnangawa kuwa alikuwa akiwauliza waganga ili kujua ni lini yeye Mugabe 93, angekufa, wakati akipanga kuchukua madaraka, gazeti la serikali la Herald lilisema.

Bwana Mnangawa kwanza alisambaza uvumi kuwa rais alipanga kustaafu mwezi Machi lakini baada ya kugundua kuwa hilo halikufanyika, alianza kuwauliza waganga kuhusu ni lini nitakufa, Bw Mugabe alisema.

Wakati mmoja aliambiwa kuwa atakufa kabla ya mimi.

Akiwahutubia maelfu ya wafuazi kwenye mji mkuu Hararare, Bw Mugabe alisema kuwa Mnangawa alikosa maadili na alijaribu kuanzisha uasi kwenye chama tawala cha Zanu-PF.

Siku ya Jumatatu Mugabe alimfuta Mnangawa, mshirika wa karibu wake tangu vita vya uhuru vya miaka ya sabini, katika kile wadadisi wanasema kuwa ni njia ya kumwezesha mke wake Grace kuchukua madaraka wakati wakakufa au kustaafu.

Exit mobile version