Muungano wa Vyama vikuu vya upinzani nchini Kenya (NASA) vyamtangaza Raila Odinga kuwania nafasi ya Urais.

In Kimataifa

Muungano wa vyama vikuu vya upinzani nchini Kenya umetaja mgombea wake wa urais atakaepambana na Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu wa Agosti.
Muungano huo unaojulikana kama The National Super Alliance (NASA), ulimtangaza waziri mkuu wa zamani Raila Odinga kuwania nafasi ya rais, na makamu wa zamani wa rais Kalonzo Musyoka kuwa mgombea mwenza wake.
Odinga alisema ikiwa atachaguliwa atapambana dhidi ya rushwa, ambayo ni mmoja ya matatizo makuu yanayolikabili taifa hilo.
Kenyatta aliwashinda Odinga na Kalonzo mwaka 2013 kwa asilimia 50.07 ya kura, kukiwa na tofauti ya kura 4,099 kati yao, hali iliompelekea Odinga kupinga matokeo hayo mahakamani.
Kenyatta ni mtoto wa Rais wa kwanza wa Kenya Jomo Kenyatta, na Odinga ni mtoto wa makamu wa kwanza wa rais Jaramogi Oginga Odinga.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu