Muungano wa Vyama vikuu vya upinzani nchini Kenya (NASA) vyamtangaza Raila Odinga kuwania nafasi ya Urais.

In Kimataifa

Muungano wa vyama vikuu vya upinzani nchini Kenya umetaja mgombea wake wa urais atakaepambana na Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu wa Agosti.
Muungano huo unaojulikana kama The National Super Alliance (NASA), ulimtangaza waziri mkuu wa zamani Raila Odinga kuwania nafasi ya rais, na makamu wa zamani wa rais Kalonzo Musyoka kuwa mgombea mwenza wake.
Odinga alisema ikiwa atachaguliwa atapambana dhidi ya rushwa, ambayo ni mmoja ya matatizo makuu yanayolikabili taifa hilo.
Kenyatta aliwashinda Odinga na Kalonzo mwaka 2013 kwa asilimia 50.07 ya kura, kukiwa na tofauti ya kura 4,099 kati yao, hali iliompelekea Odinga kupinga matokeo hayo mahakamani.
Kenyatta ni mtoto wa Rais wa kwanza wa Kenya Jomo Kenyatta, na Odinga ni mtoto wa makamu wa kwanza wa rais Jaramogi Oginga Odinga.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu