Mwalimu mkuu amcharaza viboko mwalimu mwenzake.

In Kitaifa

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Migango wilayani Biharamulo, amemchapa viboko mwalimu mwenzake mbele ya wanafunzi akimtuhumu kwa wizi wa sahani tano, pamoja na nusu kilo ya sukari iliyotolewa kwa ajili ya mahafali ya wahitimu wa darasa la saba.
Katika taarifa yake ya kulaani kitendo hicho, kaimu katibu wa Chama cha Walimu Tanzania CWT Wilaya ya Biharamulo Joseph Lugumba amesema kuwa, mwalimu mkuu Mateso Musaku alimpiga viboko mwalimu wake Hosea Masatu mbele ya wanafunzi, tukio ambalo linalaaniwa vikali.
Lugumba amesema baada ya kupata taarifa za mwalimu huyo kuchapwa viboko uongozi wa CWT ulifika shuleni hapo kujiridhisha, ambako wanafunzi na wazazi walithibitisha tukio hilo, ikidaiwa kwamba mwalimu huyo alifungwa kamba kwenye mti.
Amesema mwalimu Masatu alidaiwa kuiba vitu hivyo siku moja baada ya kumalizika mahafali ya darasa la saba, na kwamba alipoulizwa alikiri.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu