Mwalimu mkuu amcharaza viboko mwalimu mwenzake.

In Kitaifa

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Migango wilayani Biharamulo, amemchapa viboko mwalimu mwenzake mbele ya wanafunzi akimtuhumu kwa wizi wa sahani tano, pamoja na nusu kilo ya sukari iliyotolewa kwa ajili ya mahafali ya wahitimu wa darasa la saba.
Katika taarifa yake ya kulaani kitendo hicho, kaimu katibu wa Chama cha Walimu Tanzania CWT Wilaya ya Biharamulo Joseph Lugumba amesema kuwa, mwalimu mkuu Mateso Musaku alimpiga viboko mwalimu wake Hosea Masatu mbele ya wanafunzi, tukio ambalo linalaaniwa vikali.
Lugumba amesema baada ya kupata taarifa za mwalimu huyo kuchapwa viboko uongozi wa CWT ulifika shuleni hapo kujiridhisha, ambako wanafunzi na wazazi walithibitisha tukio hilo, ikidaiwa kwamba mwalimu huyo alifungwa kamba kwenye mti.
Amesema mwalimu Masatu alidaiwa kuiba vitu hivyo siku moja baada ya kumalizika mahafali ya darasa la saba, na kwamba alipoulizwa alikiri.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu