Mwanajeshi aliyeuawa katika shambulio la kombora nchini Mali ametambuliwa leo ni mwanajeshi kutoka Liberia.

In Kimataifa

  Mwanajeshi wa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa aliyeuwawa katika shambulio la kombora lililodaiwa na muungano wa wapiganaji jihadi nchini Mali ametambuliwa leo na umoja huo kuwa ni mwanajeshi kutoka Liberia.

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa unaofahamika kama MINUSMA uliwekwa katika nchi hiyo ya Afrika magharibi tangu mwaka 2013 na unachukuliwa kuwa ujumbe hatari kabisa wa umoja huo unaofanyakazi ya kulinda amani.

Ujumbe huo wa MINUSMA umesema wanajeshi wengine wanane walijeruhiwa na shambulio hilo la kombora katika kambi yao katika mji wa kihistoria wa Timbuktu Jumatano mchana.

Liberia ina wanajeshi 78 wanaotumikia katika kikosi chenye wanajeshi 13,000 wa MINUSMA ambacho kinasaidia majeshi ya Mali yanayojaribu kuweka usalama nchini humo.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu