Mwanajeshi aliyeuawa katika shambulio la kombora nchini Mali ametambuliwa leo ni mwanajeshi kutoka Liberia.

In Kimataifa

  Mwanajeshi wa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa aliyeuwawa katika shambulio la kombora lililodaiwa na muungano wa wapiganaji jihadi nchini Mali ametambuliwa leo na umoja huo kuwa ni mwanajeshi kutoka Liberia.

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa unaofahamika kama MINUSMA uliwekwa katika nchi hiyo ya Afrika magharibi tangu mwaka 2013 na unachukuliwa kuwa ujumbe hatari kabisa wa umoja huo unaofanyakazi ya kulinda amani.

Ujumbe huo wa MINUSMA umesema wanajeshi wengine wanane walijeruhiwa na shambulio hilo la kombora katika kambi yao katika mji wa kihistoria wa Timbuktu Jumatano mchana.

Liberia ina wanajeshi 78 wanaotumikia katika kikosi chenye wanajeshi 13,000 wa MINUSMA ambacho kinasaidia majeshi ya Mali yanayojaribu kuweka usalama nchini humo.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu