Mwanajeshi wa Ufaransa auawa nchini Mali katika mapigano na waasi

In Kimataifa

Mwanajeshi wa Ufaransa ameuawa usiku wa kuamkia siku ya Alhamisi nchini Mali.

Ripoti zinasema kuwa, mauaji haya yalijiri baada ya wanajeshi wa Ufaransa kukabiliana na waasi Kusini Mashariki mwa nchi hiyo.

Ikulu ya Ufaransa, Elysee, imethibitisha kifo cha mwanajeshi huyo.

Rais Francois Hollande amesema  mwanajeshi huyo anayefahamika kama Julien Barbe, amepoteza maisha akipigania usalama na amani nchini Mali, na anasalia kuwa shujaa.

Ufaransa imekuwa ikiongoza operesheni maarufu kama Serval, kuanzia mwaka 2012 kukabiliana na makundi ya waasi hasa Kaskazini mwa nchi hiyo.

Wanajeshi 17 wa Ufaransa nchini Mali katika makabiliano na waasi nchini Mali.

Mauaji haya yanakuja wakati huu Waziri Mkuu Bernard Cazeneuve akizuru nchini Algeria na baadaye Tunisia.

Naye Waziri wa Mambo ya nje Jean-Marc Ayrault anazuru Mauritania.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu