Mwanajeshi wa Ufaransa auawa nchini Mali katika mapigano na waasi

In Kimataifa

Mwanajeshi wa Ufaransa ameuawa usiku wa kuamkia siku ya Alhamisi nchini Mali.

Ripoti zinasema kuwa, mauaji haya yalijiri baada ya wanajeshi wa Ufaransa kukabiliana na waasi Kusini Mashariki mwa nchi hiyo.

Ikulu ya Ufaransa, Elysee, imethibitisha kifo cha mwanajeshi huyo.

Rais Francois Hollande amesema  mwanajeshi huyo anayefahamika kama Julien Barbe, amepoteza maisha akipigania usalama na amani nchini Mali, na anasalia kuwa shujaa.

Ufaransa imekuwa ikiongoza operesheni maarufu kama Serval, kuanzia mwaka 2012 kukabiliana na makundi ya waasi hasa Kaskazini mwa nchi hiyo.

Wanajeshi 17 wa Ufaransa nchini Mali katika makabiliano na waasi nchini Mali.

Mauaji haya yanakuja wakati huu Waziri Mkuu Bernard Cazeneuve akizuru nchini Algeria na baadaye Tunisia.

Naye Waziri wa Mambo ya nje Jean-Marc Ayrault anazuru Mauritania.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu