Mwendesha mashtaka wa kesi za ufisadi nchini Brazil amfungulia mashtaka rais.

In Kimataifa

Mwendesha mashtaka wa kesi za ufisadi nchini Brazil amemfungulia mashtaka rais Michel Temer kwa kosa la kuzuia sheria kuchukuwa mkondo wake na kuhusika katika mtandao wa rushwa.

Hatua hiyo ni ya pili katika kesi ya jinai inayomkabili rais huyo ambaye amekanusha madai hayo.

Wanamtuhumu bwana Temor kwa kuchukua hongo na kujaribu kuwanyamazisha mashahidi.
Bwana Temer amepinga madai ya kufanya makosa yoyote.

Mashtaka ya awali ya ufisadi yalizuiwa na bunge la uwakilishi ambalo lina uwezo wa kuamua iwapo rais anafaa kufunguliwa mashtaka au la.

Katika shtaka la pili rais Temer ameshtakiwa pamoja na washirika wake sita wa kisiasa.

Kiongozi wa mashtaka Rodrigo Janot amesema katika taarifa kwamba bwana Temer alihudumu kama kiongozi wa genge la wahalifu linaloshirikisha wanachama waandamizi wa chama chake cha PMDB.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu