Mwendesha mashtaka wa kesi za ufisadi nchini Brazil amfungulia mashtaka rais.

In Kimataifa

Mwendesha mashtaka wa kesi za ufisadi nchini Brazil amemfungulia mashtaka rais Michel Temer kwa kosa la kuzuia sheria kuchukuwa mkondo wake na kuhusika katika mtandao wa rushwa.

Hatua hiyo ni ya pili katika kesi ya jinai inayomkabili rais huyo ambaye amekanusha madai hayo.

Wanamtuhumu bwana Temor kwa kuchukua hongo na kujaribu kuwanyamazisha mashahidi.
Bwana Temer amepinga madai ya kufanya makosa yoyote.

Mashtaka ya awali ya ufisadi yalizuiwa na bunge la uwakilishi ambalo lina uwezo wa kuamua iwapo rais anafaa kufunguliwa mashtaka au la.

Katika shtaka la pili rais Temer ameshtakiwa pamoja na washirika wake sita wa kisiasa.

Kiongozi wa mashtaka Rodrigo Janot amesema katika taarifa kwamba bwana Temer alihudumu kama kiongozi wa genge la wahalifu linaloshirikisha wanachama waandamizi wa chama chake cha PMDB.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu